Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Mkuu akereka kuzorota mradi wa Afya

Majaliwa Web Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Fri, 27 Aug 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, hajaridhishwa na ujenzi wa Hospitali ya mkoa wa Katavi ambao ulianza tangu 2018 na hadi sasa umekamilika kwa asilimia 48 pekee na kumuagiza Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel, kubaki mkoani humo ili kubadilisha mfumo wa ujenzi wa hospitali hiyo.

Ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea Mradi huo wa maendeleo mapema hii leo, na kukuta mapunufu makubwa ya kiutendaji yaliyopelekea kuzorota kwa ujenzi wa hospitali hiyo.

Aidha, amewataka wakazi wanaoishi katika maeneo ya karibu na mradi huo kuimarisha ulinzi na usalama ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za watu wanaoingia bila kufuata utaratibu katika mradi huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live