Thu, 23 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Watoto wanne wamezaliwa usiku wa kuamkia leo kwenye mkesha wa Eid al Haji, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Taarifa iliyotolewa na hospitali hiyo leo Agosti 21 imeeleza kuwa kati ya watoto hao, wa kike ni wawili na wa kiume ni wawili.
“Watoto wote wamezaliwa kwa njia ya kawaida na kinamama wanaendelea vizuri,” imesema taarifa hiyo.
Chanzo: mwananchi.co.tz