Fri, 24 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Tabora.Watu watano wa família moja wamelazwa hospitali ya wilaya ya Urambo baada ya kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu.
Akizungumza leo Agosti 24 kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema tukio hilo limetokea katika kijiji cha Kamgembya, kata ya Nsenda wilayani Urambo.
Amesema wanafamilia hao watano waliolazwa hospitali ya wilaya wanaendelea vizuri na hakuna yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Chanzo: mwananchi.co.tz