Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wasichana 27 kati ya 100 hujifungua chini ya umri nchini Tanzania

Wasichana 27 kati ya 100 hujifungua chini ya umri nchini Tanzania

Thu, 28 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Kati ya wasichana 100 nchini Tanzania, 27 hujifungua wakiwa na umri chini ya miaka 18.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametoa takwimu hizo leo Jumanne Novemba 26, 2019 mjini Dodoma  katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa wanawake duniani.

Amesema idadi hiyo ni kubwa ingawa Serikali imepanga kuipunguza hadi kufikia watoto 13 Juni 22, 2020.

Waziri huyo amesema mapambano  dhidi ya mimba za utotoni bado ni makubwa kutokana na jamii kutokuwa na mwamko licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali.

"Tunataka Juni 22,2019 tuwe na asilimia 13.5 kutoka  asilimia 27, lazima tusimamie mila na desturi zetu zinazopinga  ukatili wa wanawake tukiwashirikisha wazee na viongozi wa dini katika maeneo yetu," amesema Ummy.

Waziri huyo amewataka viongozi kuiga mfano  wa mkuu wa Mkoa wa Tabora,  Aggrey Mwanri ambaye ni kinara wa mapambano  ya ndoa za utotoni kwa kauli mbiu yake ya ‘sukuma ndani’.

Chanzo: mwananchi.co.tz