Dar es Salaam. Biashara ya juisi ya miwa inazidi kushamiri katika maeneo ya mikusanyiko ya watu, kama vituo vya mabasi na masoko.
Licha ya juisi hiyo kutajwa kuwa na faida kwa mwili wa binadamu, watumiaji wanapaswa kuzingatia usalama wao kabla ya kuitumia.
Hii ni kutokana na watengenezaji wengi kutozingatia usafi katika maeneo yao ya biashara, mwili, mavazi au vifaa. Pia baadhi huhifadhi miwa sehemu ambayo si salama kwa afya.
“Kwa kweli napenda juisi ya miwa, lakini lazima nimkague kwanza mtengenezaji kama amevaa glovu, jinsi anavyoweka miwa na hata vyombo anavyotumia,” anasema Martha John, mkazi wa Tabata Kinyerezi.