Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

‘Wanywaji juisi ya miwa chukueni tahadahari’

78667 Miwa+pic

Mon, 7 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Biashara ya juisi ya miwa inazidi kushamiri katika maeneo ya mikusanyiko ya watu, kama vituo vya mabasi na masoko.

Licha ya juisi hiyo kutajwa kuwa na faida kwa mwili wa binadamu, watumiaji wanapaswa kuzingatia usalama wao kabla ya kuitumia.

Hii ni kutokana na watengenezaji wengi kutozingatia usafi katika maeneo yao ya biashara, mwili, mavazi au vifaa. Pia baadhi huhifadhi miwa sehemu ambayo si salama kwa afya.

“Kwa kweli napenda juisi ya miwa, lakini lazima nimkague kwanza mtengenezaji kama amevaa glovu, jinsi anavyoweka miwa na hata vyombo anavyotumia,” anasema Martha John, mkazi wa Tabata Kinyerezi.

Kwa undahi wa habari hii pata nakala ya Gazeti la Mwananchi, Jumapili ya Octoba 6.

Chanzo: mwananchi.co.tz