Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanaotumia simu, kompyuta wapewa tahadhari

50790 Pic+afya+simu

Sun, 7 Apr 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wanaotumia vifaa vya mawasiliano ikiwamo kompyuta, simu, tableti wametakiwa kutumia lenzi maalumu ili kujikinga na mionzi inayoathiri macho.

Hayo yamesemwa leo Jumamosi Aprili 6, 2019 na mkurugenzi wa kliniki ya macho ya Karibu Eye Center, Abdillah Dada, kwenye kambi maalumu ya upimaji afya iliyoandaliwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL).

MCL inazalisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen, MwanaSpoti na MCL Digital

Dada amesema watoto wa miaka kuanzia mitano hadi 16 ndiyo sana wanaosumbuliwa na tatizo sana la macho kwa siku za hivi karibuni.

Amesema hiyo inatokana na wengi wao kutumia vifaa vya mawasiliano muda mrefu ikiwamo simu, kompyuta bila kuweka vifaa vya kuzuia mionzi.

"Wazazi mtoto akifikisha miaka mitano na kuendelea anajitegemea na anaanza kujifunza au kutumia vifaa hivyo, bila uangalizi hadi atakapoanza kulalamika kuumwa macho au kutoona vizuri ndiyo anakwenda kupimwa.”

Related Content

"Ushauri wangu watumie vikinga mionzi na wapime macho mara kwa mara, wasisubiri hadi mtoto au kijana aanze kulalamika kuhusu macho," amesema Dada.

Dada ameeleza kwenye kliniki yao ya Karibu Eye Center wanaagiza vifaa hivyo kutoka nchini Uturuki vyenye ubora wa hali ya juu.

"Kwenye kambi hii iliyoandaliwa na Mwananchi tunapima macho, tunatoa fremu, tunapokea bima mbalimbali na tunatoa ushauri" amesema Dada na kufafanua kuwa wanatumia mashine za kisasa kutoa huduma ya macho.



Chanzo: mwananchi.co.tz