Akizungumzia changamoto hiyo ya uhaba wa matundu ya vyoo Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Vick Laizer, amesema tatizo hilo limedumu kwa muda mrefu.
Kutokana na changamoto hiyo, wadau wa elimu kutoka katika Shirika la Sos Children’s Villages limetoa msaada wa mifuko 50 ya saruji pamoja na mchanga tani 18 kwa ajili ya ujenzi wa choo kipya.
Wakikabidhi msaada huo Shirika hilo limesema litaendelea kumuenzi aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dk. John Magufuli kwa kuhakikisha kuwa wanaendelea kuwasaida watoto wanaotoka kwenye mazingira magumu ili dhamira yake ya kuhakikisha elimu inawafikia wote.