Hamasa imetolewa kwa walimu visiwani Zanzibar kutoa ushauri mzuri kwa wanafunzi utakawasaidia kuwaongoza kwenye maisha yao ikiwemo kufahamu namna nzuri ya kujikinga na maambukizi mapaya ya Virusi vya Ukimwi (VVU).
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Dk Idrissa Muslimu Hija alipokuwa anafungua mafunzo ya afya ya uzazi, jinsia pamoja na Ukimwi kwa walimu wa madrasa ya Msingi na kati na sekondari mjini Unguja.
“Mnatakiwa kutoa ushauri kwa upole kwa wanafunzi wenu ili waweze kujikinga na maambukizi mapaya ya virusi vya Ukimwi ili wawe na weledi wa kutosha ni namna gani wanaweza kupambana na ugonjwa huo,” amesema Hija.