Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wagonjwa wenye matatizo ya afya ya akili waongezeka kwa kasi

Afya Ya Akili Pic 780x470 Wagonjwa wenye matatizo ya afya ya akili waongezeka kwa kasi

Sat, 7 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Mwananyamala imeripoti ongezeko la wagonjwa wa matatizo ya afya ya akili kutoka wastani wa watu watano hadi nane awali mpaka kufikia wastani wa 30 hadi 45 kwa siku.

Hayo yameelezwa na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Zavery Benela wakati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam katika Wiki ya Afya ya Akili ambapo amesema ongezeko hilo la wagonjwa linatokana na visababishi mbalimbali vikiwemo vya kibaiolojia, kisaikolojia na kimazingira jambo ambalo amesema linahitaji wataalamu ili kulidhibiti.

“Kuanzia Juni mwaka jana, tumeanza kupata ongezeko kubwa la wagonjwa wa aya ya akili ambalo linafikia wagonjwa 30 mpaka 45 kwa siku. Kabla tulikuwa tunapata wagonjwa watano mpaka wanane kwa siku, jambo linaloonesha uhitaji wa kuwapo wataalamu wa magonjwa ya afya ya akili katika hospitali zetu,” ameeleza.

Kutokana na ongezeko hilo, Dkt. Benela ametoa wito kwa wataalamu wa fani za udaktari kusoma pia udaktari wa afya ya akili kwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa wataalam hao kwa sasa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live