Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wabunge waibua mjadala Hospitali ya Mirembe kujengwa Dodoma, Serikali yatoa ufafanuzi

52983 MILEMBE+PIC

Fri, 19 Apr 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Serikali ya Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu sababu za kujengwa kwa hospitali ya magonjwa ya akili ya Mirembe jijini Dodoma kuwa haikutokana na mkoa huo kuwa na wagonjwa wengi.

Majibu hayo yametolewa leo Alhamisi Aprili 18, 2019 wakati wabunge walipojadili kuhusu masuala ya magonjwa ya akili swali ambalo liliibua mjadala kwa wabunge.

Akijibu swali hilo ambalo Spika wa Bunge, Job Ndugai alikuwa ameliuliza kama utani, akisema mitandao mingi ilikuwa inazungumzia kwa nini maeneo mengine imejengwa miradi wakati Dodoma kuna hospitali ya magonjwa ya akili.

"Si kweli kuwa Dodoma kuna wagonjwa wengi wa akili lakini hospitali ya Mirembe ni hospitali ya rufaa iliyojengwa kwa sababu ya kuwapo wa Gereza Kuu la Isanga ambalo linapokea watu wenye kesi kubwa hivyo huweza kupata msongo (wa mawazo)," amesema Dk Ndugulile.

Katika swali la msingi Mbunge wa Njombe (CCM, Edward Mwalongo aliuliza kama Serikali inawahudumia wagonjwa wa akili wanaozurura mitaani katika masuala ya matibabu, mavazi na makazi.

Naibu waziri amesema Serikali imeendelea kuimarisha afya ya akili kuanzia ngazi za juu hadi ngazi ya msingi ambako jamii inatoka.

Amesema pamoja na idadi kubwa ya wagonjwa wanaorandaranda mitaani, bado huduma zinatolewa lakini akasema sheria ya afya ya akili ya mwaka 2008 inawataka ndugu na jamii kuibua wagonjwa wa akili na kuwapeleka kupata matibabu.



Chanzo: mwananchi.co.tz