Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vituo 100 vya Afya vyaboreshwa Kigoma

Mon, 24 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mkoa wa Kigoma umenufaika na mradi wa Afya ya Mama na Mtoto mradi uliofanikisha kuboresha vituo vya afya 100.

Mradi huo ambao umedhaminiwa na Meya wa Marekani, Michael Bloomberg kupitia Taasisi ya Bloomberg Phalanthropies ya New York City kwa kushirikiana na Taasisi za Thamini Uhai, Engender Health na H&B Agerup, ulianzishwa mwaka 2006 katika mikoa ya Kigoma, Pwani na Morogoro.

Dk Godson Maro ambaye ni mratibu wa Afya ya mama na mtoto kutoka Taasisi ya Bloomberg, ameliambia Mwananchi leo Jumapili Juni 23,2019 kuwa awali Mkoa wa Kigoma ulikuwa na changamoto nyingi za afya ya mama na mtoto hasa ya wazazi wengi kujifungulia nyumbani.

“Kupitia mradi huu sasa, zaidi ya watoto 210,000 wamezaliwa kwenye vituo vya afya vilivyoboreshwa,” amesema Maro.

Amesema Serikali ya Tanzania ilikuwa na maono ya kupeleka huduma za kuokoa maisha ya mjamzito maeneo ya pembezoni kuliko na changamoto nyingi na kwa Kigoma imefanikiwa.

Maro amesema mkoani Kigoma mradi huo umeboresha kwenye vituo vya afya 100 ambavyo ni hospitali tatu, vituo vya afya 13 na zahanati 82 kwa kusaidia upatikanaji wa dawa muhimu, vifaa tiba na vitendea kazi.

Pia Soma

“Mradi ulihusisha mikoa mitatu nchini, lakini Kigoma ilipewa kipaumbele zaidi kutokana na changamoto ya vifo vingi vilivyotokana na uzazi ambavyo kwa sasa vimepungua,” amesema Maro.

Amesema licha ya mradi huo kufikia tamati, lakini umeacha huduma katika mkoa huo zikiendelea ikiwamo matumizi ya uzazi wa mpango ambao umetoka asilimia 15.6 mwaka 2014 na kufikia asilimia 21 mwaka jana.

Chanzo: mwananchi.co.tz