Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Utayari kukabiliana na Ebola waanza Kigoma

70051 Pic+ebola

Mon, 5 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Kigoma. Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya waziri Mkuu Sera, Utaratibu na Bunge  na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendesha shughuli ya utayari wa kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini humo.

Akizungumza leo Jumatatu Agosti 5, 2019 na wadau wa afya mjini Kigoma, Mkurugenzi msaidizi utafiti na mipango idara ya menejimenti na maafa ofisi ya waziri Mkuu, Bashilu Taratibu amesema shughuli hiyo itafanyika kwa siku tano katika halmashauri tano za mkoa huo.

"Kwa awamu ya kwanza shughuli hii inafanyika kwa mikoa miwili wa Kagera ambapo tayari tumeshamaliza na sasa tupo mkoani Kigoma katika halmashauri ya Uvinza, Buhigwe, Manispaa ya Kigoma ujiji, halmshauri ya wilaya ya Kigoma na Kasulu," amesema Taratibu.

Amesema shughuli hiyo imejikita katika kuwafanyia majaribio wadau hao wa afya ambao tayari walishapata mafunzo lengo ni kuona jinsi watakavyokabiliana na mgonjwa wa Ebola akiingia nchini.

Awali, akifungua shughuli hiyo kwa niaba ya Katibu tawala mkoa Rashidi Mchatta, katibu tawala msaidizi, Daniel Machunda amesema nchi za jirani ya Demokrasia ya Congo (DRC), bado inakabiliwa na ugonjwa wa ebola tangu Agosti 2018.

Amesema  mpaka kufika Julai 31, 2019, wagonjwa 2,973 wamepata ugonjwa huo huku vifo vikiwa 1,823 ikiwa ni asilimia 68 ya idadi ya watu waliopata ugonjwa huo.

Pia Soma

Ofisa afya mwandamizi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Remidius Kakulu amesema shughuli kubwa ni kuhakikisha mipaka ambayo ipo rasmi inadhibitiwa huku viongozi wa ngazi ya kijiji kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha wanasimamia mipaka isiyo rasmi ili kuzuia ugonjwa wa Ebola kuingia nchini.

Chanzo: mwananchi.co.tz