Thu, 30 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kukwete (JKCI) imekuja na teknolojia mpya ambayo inamfanyia upasuaji mgonjwa wa moyo bila ya kumuongezea damu kama ilivyokuwa inafanyika awali.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa taasisi Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi, amesema teknolojia hiyo ambayo tayari wameanza kuitumia kwa wagonjwa itamaliza changamoto ya kukosekana Kwa damu zilizokuwa zinahitajika kwa wagonjwa kabla ya kuwafanyia upasuaji huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live