Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ummy Mwalimu akerwa na vigodoro

13793 Ummy+pic TanzaniaWeb

Sat, 25 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga.Waziri wa Afya Maendeleo ya jamii Jinsia wazee na watoto,Ummy Mwalimu  amesema anakerwa na mtindo wa baadhi ya wanafunzi wa shule za Sekondari Jijini hapa kuhudhuria ngoma za vigodoro na wengine kuvuta

bangi badala ya kujikita kwenye masomo.

 Amewataka kutumia muda wao katika masomo kwa kuwa ndiyo msingi wa maisha yao na mambo ya vigodoro pamoja na kuvuta bangi wawaachie ambao wako nje ya masomo.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo  Agosti 25  wakati akikabidhi madawati 45 yenye thamani ya Sh 5.7 milioni kwa shule ya Sekondari Toledo iliyopo kata ya Mwanzange Jijini Tanga.

“Inanitia simanzi sana kusikia  mwanafunzi anakwenda kukesha kwenye vigodoro badala ya kujisomea..niwaambieni tu kwamba kwa mtindo huo alama za ziro kwenye mitihani ya kitaifa zitazidi kuongezeka huku wenzenu wa maeneo mengine wakifika mbali kwa sababu ya juhudi ya

masomo”amesema Ummy.

Amesema katika kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi wa jijini Tanga unaongezeka ameanzisha tuzo maalumu itakayoshindaniwa na wanafunzi wa kidato cha pili watakaofaulu mitihani itakayotungwa kwa ajili ya

kuwapima viwango vyao.

Amesema tuzo hizo zitakazojulikana kwa jina la “Ummy Mwalimu Award” zitatolewa katika maeneo matatu ambayo ni  kwa mwanafunzi atakayeongoza masomo yote katika mashindano hayo,  ya pili itahusisha wasichana peke yao na    ya tatu ni kwa walimu ambao watatoa mwanafunzi

atayaeongoza mitihani hiyo.

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz