Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ujenzi kituo cha afya wilayani Hai kuwanufaisha wananchi 19,000

88489 Kituo+pic Ujenzi kituo cha afya wilayani Hai kuwanufaisha wananchi 19,000

Sat, 14 Dec 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Hai. Wananchi wa Tambarare wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wataondokana na kero ya huduma za afya baada ya Mkuu wa wilaya hiyo, Lengai Ole Sabaya kuzindua ujenzi wa kituo cha afya  kijiji cha Longoi.

Kituo hicho kinachojengwa kwa nguvu za wananchi, wadau kutoka vyama vya ushirika na Halmashauri ya Wilaya ya Hai kitatoa huduma kwa  wananchi zaidi ya 19,000 wa kata tatu.

Akizindua ujenzi huo jana Desemba 13, 2019 Sabaya amesema fedha za ujenzi wa kituo hicho cha afya zimechangwa na vyama vya ushirika, kwamba wananchi watakaonufaika ni wa kata ya Masama Rundugai, Weruweru na Mnadani.

"Fedha za ujenzi wa kituo hiki zimetokana na asilimia 50 ya mapato ya vyama vya msingi  vya wilaya hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19, fedha hizo zilileta msuguano lakini tunashukuru zimepatikana na kazi imeanza," amesema Sabaya.

Amesema tayari zaidi ya Sh338 milioni zimepatikana, kwamba zinatosha katika ujenzi wa  jengo la wagonjwa wa nje, mama na mtoto na maabara.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hai,  Dk Irene Haule amesema  upungufu wa vituo vya afya katika wilaya hiyo  ni asilimia 65.

Chanzo: mwananchi.co.tz