Tue, 11 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watafiti wa Imperial College of London wamebaini watu wenye 'T-Cells' nyingi wana uwezekano mdogo wa kupata Virusi vya Corona. T-Cells ni kati ya seli nyeupe za damu ambazo husaidia kuleta kinga mwilini
Wamebaini Mwili unapokuwa umeathiriwa na aina nyingine ya Virusi kama kwenye mafua ya kawaida, huzalisha kiasi kikubwa cha 'T-Cells' na kuulinda mwili dhidi ya COVID-19
Hata hivyo, watafiti hao wamesema namna sahihi ya kujikinga na Corona ni kupata chanjo kamili na 'Booster'
Chanzo: www.tanzaniaweb.live