Tue, 11 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Utafiti uliofanywa na Wanasayansi wa Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Saratani, IARC umebaini pombe kali ya gongo inayotengenezwa nchini Tanzania, Chang'aa ya Kenya na Kachasu ya Malawi zinasababisha Saratani ya Tumbo hususani kwa Wanaume
Utafiti ulihusisha watu 1,279 waliolazwa wakiugua Saratani ya Tumbo na 1,346 wasiougua Saratani nchini Tanzania, Malawi na Kenya. Walichunguzwa aina za pombe za kienyeji walizotumia
Mwaka 2020 Saratani ya Tumbo ilisababisha vifo vya watu 544,076 duniani. Saratani hiyo ni nadra Afrika Magharibi ilihali imeshamiri Kusini na Mashariki mwa Afrika
Chanzo: www.tanzaniaweb.live