Hospitali ya Mji wa Bariadi-Somanda imepokea mashine ya kupimia wajawazito ‘Ultrasound’ yenye thamani ya shilingi milioni 30 kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu (UNFPA).
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga amesema kupatikana kwa kifaa hicho kitarejesha huduma za upimaji kwa akina mama wajawazito na kulishukuru shirika hilo kwa msaada huo.
Aidha, Kiswaga amewataka watumishi wa hospitali hiyo kuongeza umakini katika matumizi na utunzaji wa vifaa tiba katika hospitali hiyo ili huduma ya upimaji wa magonjwa na vitu mbalimbali vya kitiba zisiweze kusimama.