TANZANIA imetajwa kuwa miongoni mwa nchi saba kinara barani Afrika katika mapambano ya Kifua Kikuu.
Mpango Mkakati wa tano uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) umebainisha kuwa Tanzania imefanikiwa kwa kiwango kikubwa katika malengo ya mwaka 2020 ya kidunia.
Nchi nyingine zilizotajwa kukabiliana na ugonjwa huo ni Kenya, Afrika Kusini, Burkina Faso, Nigeria na Msumbiji.
Dokta Zuwena Kondo, Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Idara ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) anasema Tanzania imefanikiwa kutokana na kuimarishwa kwa upatakanaji wa takwimu za wagonjwa kwa kutumia wataalamu wa ndani ya nchi hivyo kuwezesha uendelevu wa mfumo huo.
“Mfuko wa dunia wa kupambana na ukwimwi TB na Malaria umetambua mfumo huu wa ‘DHIS2TL – Tracker Module ‘ kuwa ni wa kwanza kufanikiwa katika nchi za AFrika ni bora na wa kuigwa