Sat, 3 Feb 2018
Chanzo: bongo5.com
Taasisi ya Imetosha kwa kushirikiana na Hospital ya Ocean Road imewafanyia uchunguzi watu wenye matatizo ya ngozi (Albino) zaidi ya mia moja.
Akiongea na Bongo5, mratibu wa zoezi hilo Mr, Mdimu amebaisha kuwa mpaka sasa wamepokea watu zaidi ya mia moja waliokuja kufanyiwa uchunguzi wa saratani ya ngozi.
“Tumepokea watu zaidi ya mia moja mpaka sasa na tunategemea kupata watu zaidi maana zoezi hili ni leo na kesho. Hivyo ni vyema watu wenye uhitaji wa matibabu wakafika Hospitalini hapa kuonana na wataalamu wa masuala ya ngozi waweze kuwapatia matibabu na ushauri.”
Chanzo: bongo5.com