SHIRIKA la Afya Duniani, WHO limesema idadi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na COVID-19 vimeendelea kupungua ulimwenguni katika wiki iliyopita.
WHO imesema leo Septemba 22, kuwa zaidi ya visa milioni 3.6 na vifo chini ya 60,000 vimeripotiwa kati ya Septemba 13 na 19, Kupungua kwa kiasi kikubwa cha visa hivyo kumeripotiwa kwenye nchi za Mashariki mwa Mediterania na Kusini Mashariki mwa Asia.
Aidha India imetangaza kuwa itaanza kutoa chanjo ya virusi vya corona kwa watoto wenye umri wa miaka 12 au zaidi kuanzia mwezi ujao.
Urusi kwa upande wake imetangaza kuwa takriban watu milioni 40 nchini humo wamepata chanjo kamili ya COVID-19.