Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TIBA MBADALA: Tezi dume inatibika kwa dawa za asili pia

58080 Pic+tezi+dume

Fri, 17 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Maambukizi ya tezi dume yameongezeka miaka ya hivi karibuni tofauti na zamani ilipokuwa nadra kusikia mtu amepata tatizo hili.

Wachache walio-kuwapo ni watu wazima. Wakati hamasa ya kupima ikiongezeka, changamoto mpya nazo zinaibuka. Iliyopo sasa ni gharama kubwa za matibabu yake.Matibabu ni ghali na mara nyingi wagonjwa hushauriwa kufanyiwa upasuaji ambao gharama zake hazishikiki pia hasa kwa wenye kipato cha chini.

Mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa tezi dume, wata-alamu wanasema huhitajika kurudia tena baada ya miaka mitano hivi. Lakini, ipo njia nyingine ya kukabiliana na maradhi haya nayo ni tiba mbadala. Kwa kutumia dawa za asili, tatizo hili linaweza kwisha endapo mgonjwa atafuata masharti bila kufanyiwa upasuaji, tena kwa gharama nafuu. Wataalamu wa afya ya figo na kibofu cha mkojo wanasema uvimbe usio wa saratani ambao husababisha tezi dume kupanuka ndio unaosababisha ugonjwa huu ambao huwapata wanaume tu.

Uvimbe huu ukiongeze-ka au kutanuka hasa kwa wanaume wenye zaidi ya miaka 60, hutatiza kukojoa hivyo dalili za ugonjwa huu unazidi kuongezeka duniani kuwa dhahiri.Tezi dume ni kiungo kido-go na sehemu ya uzazi wa wanaume inayopatikana chi-ni ya kibofu, mbele ya njia ya mkojo. Tezi dume ndiyo hutoa maji yabebayo mbegu (manii) za kiume.

Kupanuka kwa tezi dume ni tatizo la kawaida ambalo halisababishwi na saratani bali kadri umri unavyosogea ndivyo nalo linavyozidi kuwa kubwa hivyo kusababisha kufinya njia ya mkojo.Dalili za kupanuka kwa tezi dume huonekana baa-da ya kuanzia miaka 50 na wanaume wengi wenye kati ya miaka 70 na 80 huwa na tatizo hili.Dalili zake ni kukojoa mara

MBADALAnyingi hasa nyakati za usiku, mkojo kutoka taratibu, mkojo kushidwa kuto-ka na matone ya mkojo huendelea kuto-ka hata baada ya muhusika kumaliza kutoa haja.Pamoja na haya yote, zipo namna za kukabiliana na maradhi haya bila ghara-ma kubwa.

Pia Soma

Njia nzuri na salama kutibu tezi dume ni kutumia tiba mbadala.

Tiba hii hupatikana kwa kuchangan-ya tangawizi ya unga, kamun aswadi, khurinjani, albatisoda, hulba na sufa. Vyote viwe vya unga. Ukishavichanganya, unapaswa kutu-mia kijiko kimoja kwenye uji au chai kutwa mara tatu kwa mwezi mzima.

Chanzo: mwananchi.co.tz