Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sita wafariki dunia 361 wathibitika kuugua kipindupindu

63030 Pic+kipindupindu

Mon, 17 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Serikali imesema mpaka sasa watu sita wamefariki dunia na wengine 361 wameugua kipindupindu mwaka huu.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu Leo Juni 17, 2019, Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile amesema hali iliyopo sasa inaridhisha kwa sababu wagonjwa wanaendelea kupungua.

“Wiki mbili nyuma kimeibuka kipindupindu katika jiji la Dar es Salaam, lakini kwa sasa hali inaanza kuwa nzuri wagonjwa wanapungua na ukifika kwenye kambi za Temeke, Amana na Mwananyamala utamkuta mmoja au wawili, Takwimu kwa nchi nzima watu sita wamefariki huku 361 wakiugua ugonjwa huu,” amesema Dk Ndugulile.

Aidha, alipoulizwa kuhusu hali ya homa ya dengue, amesema takwimu zinaendelea kupungua huku akisema Serikali itatoa majibu ya takwimu hizo mwishoni mwa mwezi huu.

"Ukusanyaji takwimu bado unaendelea na Wizara tutazitoa baadaye mwezi huu," amesema.

Chanzo: mwananchi.co.tz