Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yatakiwa kuhamasisha watu kuchangia figo

14741 FIGO+PIC TanzaniaWeb

Thu, 30 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Serikali imetakiwa kuweka utaratibu maalum wa

kuhamasisha watu kujitolea kuchangia figo kwa kuwa mchakato wa kupatakiungo hicho ni mgumu kwa sababu haziuzwi.

Wito huo umetolewa leo Agosti 30 na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Egid Mubofu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma mbalimbali za kibingwa zinazotolewa na Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo chuoni hapo.

Amesema hospitali hiyo imeanza kutoa huduma ya kupandikiza figo tangu Machi mwaka huu lakini mchakato wa kuzipata

figo hizo umekuwa mgumu kwa sababu haziuzwi bali zinategemea mtu

kujitolea kwa kupenda.

"Hakuna fedha yoyote inayoweza kununua kiungo cha binadamu hivyo naiomba Serikali iweke utaratibu maalum wa watu kuchangia viungo vyao kama figo kwa ajili ya kuwapa watu wengine wenye uhitaji wa viungo hivyo kwa sababu haviuzwi," amesema Profesa Mubofu.

Amesema upatikanaji figo kwa sasa unategemea ndugu kujitolea kwa

hiari hivyo kufanya nchi kuwa na wagonjwa wengi wa figo lakini

wanaojitolea ni wachache na kwamba kukiwa na utaratibu maalum wa

kuchangia viungo hivyo kutapunguza vifo vitokanavyo na maradhi ya

figo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dk

Alphonce Chandika amesema mpaka sasa hospitali hiyo imeshapandikiza figo wagonjwa wanne ambao wanaendelea vizuri na kwa sasa ina mpango wa kuwasomesha madaktari bingwa wengine kwa ajili ya kufanya upasuaji wa magonjwa ya moyo.

Amesema lengo ni kuwawezesha Watanzania wanaohitaji matibabu ya

kibingwa kuyapata hapa nchini kwa gharama nafuu tofauti na kupelekwa

nje ya nchi.

Amesema kuwa matibabu ya kupandikiza figo ndani ya nchi ni gharama nafuu ukilinganisha na ya nje ya nchi kwa kuwa huduma hii nchini ni Sh22 milioni na wakati kwa matibabu hayo hayo nje ya nchi ni zaidi ya Sh80 milioni.

Naye Daktari Bingwa wa magonjwa ya figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dk, Kessi Shija amesema kuwa serikali ikiweka utaratibu mzuri wa watu kuchangia viungo vya binadamu viungo hivyo pia vitawezekana kupatikana hadi kutoka kwa marehemu.

“Hili zoezi la kupandikiza figo linafanyika kwa mujibu wa sheria kwa kuwa linahusisha kumfanyia upasuaji mtu ambaye si mgonjwa sasa kwa

sheria hiyo hiyo kama serikali itaridhia tutaweza kuvuna figo kwa

marehemu kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa kwa ajili ya kuwapandikizia

wahitaji,” alisema Dk, Shija.

Chanzo: mwananchi.co.tz