Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yataja mifumo ya ufuatiliaji Ebola

63060 Pic+kipindupindu

Mon, 17 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wakati Kericho nchini Kenya tayari kunahisiwa kuwa na mgonjwa wa Ebola, Serikali imesema tayari imeweka mifumo ya ufuatiliaji kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi Leo Juni 17, 2019 Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile amesema katika kuhakikisha wanachukua hatua tahadhari zote zinachukuliwa ikiwemo utayari wa wataalamu wenye mafunzo ya kuhudumia wagonjwa.

Tayari kuna maeneo yametengwa kwa ajili ya kuwahifadhi wagonjwa, mifumo ya kimaabara, ufuatiliaji wa wahisiwa, na mazoezi kwa wataalamu wa afya kwa ajili ya utayari.

"Tayari vifaa maalum vimefungwa viwanja vya ndege na mipakani kuangalia kila anayeingia, wanaoenda Congo hasa madereva tuna utaratibu wa kuwafuatilia wanapoingia nchini na pia wanakwenda maeneo gani, lazima tuhakikishe tunafuatilia mnyororo nzima kwa wafanyabiashara waendelee ila wachukue tahadhari," amesema Dk Ndugulile.

Aidha ameitaka jamii itoe taarifa kwa Mamlaka husika pindi wakimbaini mhisiwa.

Chanzo: mwananchi.co.tz