Hospitali ya Kibong’oto ni miongoni mwa hospitali Kongwe zaidi nchini Tanzania , ifikapo 2026 hospitali hii itatimiza miaka 100 tangu kianzishwa kwake.
Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan bado inawekeza nguvu nyingi ili kuboresha huduma katika hospitali hii maalumu ya magonjwa yanayoambukizwa
Mkurugenzi wa hospitali hii ya Kibong’oto Leonard Subi anaeleza mambo ambayo Serikaki imefanya katika kipindi cha miaka mitatu cha uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Wasafi media tumezungumza na baadhi ya wagonjwa wanaotibiwa katika hospitali hiyo, na wao wamezungumzia huduma wanazozipata katika hospitali hiyo.