Wed, 9 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kuanzia Januari 29 hadi Februari 6, 2022 visa vipya 252 vya #COVID19 vilibainika kati ya watu 8,529 waliopimwa huku Dar es Salaam ikiongoza kwa kuwa na maambukizi 184.
Tangu Mlipuko kuripotiwa Machi 2020 hadi kufikia tarehe Februari 6, 2022 jumla ya watu 33,482 (7.6%) kati ya 442,566 waliopima walithibitika kuwa na maambukizi, 792 wamepoteza maisha.
Hadi Februari 6, 2022 dozi 9,845,774 za chanjo zilikuwa zimepokelewa Nchini, na jumla ya watu 2,117,387 (3.67%) wamepata dozi kamili tangu zoezi la utoaji chanjo kuanza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live