Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania yatoa tahadhari mlipuko wa Ebola

13013 Ebola+pic TanzaniaWeb

Tue, 21 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Serikali imetoa tahadhari kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini baada ya watu 91 kuugua DRC Congo na wengine 50 kufariki dunia.

Idadi hiyo imeongezeka kutoka wagonjwa 26 katika mlipuko uliotokea Julai mwaka huu.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Agosti 21 Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema nchi ipo hatarini kupata ugonjwa huu kwa sababu ya ujirani kati ya Congo na Tanzania lakini mpaka sasa bado haujaingia nchini Tanzania.

Ameitaja mikoa ambayo ipo hatarini kuwa ni pamoja na Mwanza, Kagera, Katavi, Rukwa na Songwe ambayo ipo mipakani.

Huo ni mlipuko wa 10 kutokea nchini DRC Congo huku  wastani wa wanaoambukizwa na wanaofariki ukitajwa kuwa ni wa  kiwango cha  asilimia 50.

Chanzo: mwananchi.co.tz