Serikali imesema ipo tayari kutoa kadi za kieletroniki kwa wachangia damu ili kuepusha usumbufu endapo watahitaji huduma kwani kadi hizo zitaonesha jina la mchangiaji damu, kundi la damu na namba ya kadi.
Haya yameelezwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu mapema Februari 25, 2022 wakati alipotembelea makuu ya damu salama jijini Dar es Salaam kuona hali ya upatikanaji wa damu nchini na kujadiliana na uongozi jinsi gani ya kutatua changamoto ya uhaba wa damu ktk vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Amebainisha kuwa kila atakayechangia damu atapewa kipaumbele akiwa na kwenye uhitaji wa damu au akiwa na mgonjwa mwenye uhitaji wa damu.