Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali kuja na mkakati huu sekta ya Afya

VFCDD.jpeg Dorothy Gwajima, Waziri wa Afya

Sun, 19 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katika hali ya kuendelea kupunguza Vifo vya Mama na Mtoto, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima, amesema kuanzia sasa kutakuwa na Utaratibu wa Mikutano kwa Njia ya Mtandao (Zoom), kila siku baina ya wataalam wa Wizara, Mkoa na Kituo kilipo tokea kifo husika, ili kubaini endapo kuna uzembe uliojitokeza katika kumhudumia mzazi au mjamzito hadi akapoteza uhai.

Dkt. Gwajima amesema, lengo la kufanya hivyo ni kutaka kubaini endapo kuna uzembe au huduma ilienda sawa hatua zote, na kama ikibainika mtoa huduma kafanya uzembe basi kitakachofuata ni mhusika au wahusika kufikishwa kwenye Mabaraza ya kitaaluma yanayosimamia taaluma husika.

Dkt. Gwajima, amesema zoezi hilo litakaloanza tarehe 20 Desemba, 2021, ni sehemu ya Mpango Mkakati wa Tano wa Sekta ya Afya uliozinduliwa Julai, 2021 ili kumsaidia mama awe na uzazi salama.

” Mimi naamini, vifo vingi vinazuilika na ukichunguza kwa undani utaona kuwa siyo vyote ni majaliwa ya Mungu bali vingine ni uzembe au kutojali kwa baadhi ya watoa huduma ambao wameshindwa kusimamia taaluma kwa misingi inayoongoza taaluma zao, hivyo kuanzia sasa tunaunda timu ngazi ya Wizara, ili kufanya Tathmini ya vifo vyote vinavyotokana na uzazi”. Amesema Dkt. Gwajima.

Katika hatua nyingine, Dkt. Gwajima, amepata fursa ya kuzungumza na Madaktari Wanafunzi waliopo Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, ambapo katika mazungumzo yao amewataka Madaktari hao, kuishi miiko inayo ongoza taaluma yao.

Awali alipokea changamoto mbalimbali za Madaktari hao wanafunzi, ambapo walipendekeza Matumizi ya Teknolojia katika uendeshaji wa shughuli za Hospitali katika wakati wa sasa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live