Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RIPOTI: Madaktari na wauguzi Afrika wanapambana na janga bila kinga ya COVID-19

Taking A Sample Swab In Kakata Liberia Madaktari na wauguzi Afrika wanapambana na janga bila kinga ya COVID-19

Fri, 26 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Imeelezwa kuwa ni mfanyakazi mmoja tu kati ya wanne kutoka sekta ya afya barani Afrika ambaye amepewa chanjo kamili dhidi ya Covid-19, na kuacha idadi kubwa ya wafanyikazi kwenye mstari wa mbele wa janga hili bila kinga, uchambuzi wa awali wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) unaonesha.

Uchambuzi wa takwimu zilizoripotiwa kutoka nchi 25 unaonesha kuwa tangu Machi 2021, wafanyakazi wa afya milioni 1.3 barani Afrika, au asilimia 27, wamechanjwa kikamilifu.

Kinyume chake, utafiti wa hivi karbuni wa kimataifa wa WHO katika nchi 22 zenye kipato kikubwa ulionyesha kuwa asilimia 80 ya wafanyakazi wao wa afya na wahudumu wa afya wameathirika na janga hilo.

"Wahudumu wengi wa afya barani Afrika bado wanakosa chanjo na wanabaki wazi kwa maambukizo makali ya Covid-19. Isipokuwa madaktari wetu, wauguzi na wafanyikazi wengine wa mstari wa mbele wapate ulinzi kamili tunahatarisha kurudi nyuma katika juhudi za kukabiliana na ugonjwa huu. Ni lazima tuhakikishe vituo vyetu vya afya ni mazingira salama ya kufanyia kazi,” alisema Dk Matshidiso Moeti, Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live