Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

RC Geita aiangukia Serikali ya Tanzania ujenzi wa chuo kikuu cha sayansi na tiba

69310 Limu+pic

Thu, 1 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Geita. Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel ameiomba Wizara ya Elimu nchini Tanzania kujenga chuo kikuu cha sayansi na tiba ya afya katika eneo inakojengwa Hospitali ya Rufaa Chato ili kuleta mapinduzi katika sekta ya afya.

Gabriel ametoa ombi hilo leo Alhamisi Agosti Mosi, 2019 katika ziara ya naibu Waziri wa Elimu, William Olenasha  kukagua miradi ya elimu inayotekelezwa wilayani Geita.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kujengwa kwa chuo katika eneo hilo kutasaidia kuinua motisha katika mkoa huo ambao ulichelewa kuwa na vyuo kutokana na jamii kuwa na mwamko mdogo wa elimu

Akizungumzia ombi Olenasha amesema wazo la kuwa na chuo cha sayansi na tiba ni jambo jema kutokana na nchi kuwa na upungufu wa vyuo vya sekta ya afya.

Ameutaka uongozi wa Mkoa kuendelea na mchakato wa kutafuta ardhi kwa ajili ya ujenzi huku yeye alipeleka wazo hilo wizarani kuona namna ya kulifanya.

Akikagua ujenzi wa jengo udhibiti ubora wa elimu linalojengwa katika halmashauri ya Geita kwa gharama ya Sh150 milioni, Olenasha  amesema wizara yake imetoa Sh760 milioni kwa ajili ya majengo 100 nchi nzima.

Pia Soma

Amesema lengo ni kuwezesha idara ya udhibiti ubora kufanya kazi na kusimamia ubora wa elimu inayotolewa nchini, kwamba  mbali na ujenzi wa majengo pia Serikali imetoa magari 45 na pikipiki kwa maofisa elimu kata nchi nzima.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz