Mon, 18 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
WALAJI wa Nyama ya Nguruwe wapo hatarini kutokana na kuzuka kwa homa ya Nguruwe (Afircan Swine Fever) katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Annamringi Macha amepiga marufuku biashara ya nyama hiyo ya Nguruwe na uuzaji wa nguruwe wenyewe kutokana na ugonjwa huo.
Imeelezwa kuwa toka kuzuka kwa homa hiyo nguruwe zaidi ya 500 wamekufa.
Akizungumza, Mkuu huyo wa wilaya amesema amechukua uamuzi huo ili kuwakinga wananchi na watumiaji wa kitoweo hicho na madhara ya ugonjwa huo Swine.
Chanzo: habarileo.co.tz