Wed, 25 Nov 2020
Chanzo: habarileo.co.tz
Imeelezwa kuwa tatizo la mafua yasiyopona linatokana na mzio ‘allergy’.
Hayo yamesemwa na Dk Abraham Mwakalambo wa Zahanati ya Mkolemba, wilayani Ilala, Dar es Salaam na kushauri mtu anayesumbuliwa na tatizo hilo afanye kipimo cha mzio ili kujua ni kitu gani kinachomsababishia ugonjwa huo.
Amesema ugonjwa wa mafua unaweza kumasababishia mtu kupata ‘pneumonia’ na kupoteza kabisa uwezo wa kuhisi harufu.
Chanzo: habarileo.co.tz