Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muhimbili yampokea Mbowe

9464 Mboeee+pic TZWeb

Mon, 18 Jun 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Aminiel Aligaesha amesema Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe alipokelewa hospitalini hapo leo asubuhi.

Akizungumza na MCL Digital leo Juni 18, Aligaesha amesema: “Ni kweli tumempokea Mbowe leo asubuhi.”

Soma Zaidi: Freeman Mbowe adondoka ghafla, alazwa Muhimbili

Awali, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilielezwa kuwa, Mbowe ameshindwa kufika mahakamani baada ya kuanguka ghafla akiwa nyumbani kwake.

Wakili wake, Jeremiah Mtobesya aliiambia Mahakama leo kuwa mteja wake ameshindwa kufika mahakamani baada ya kuanguka ghafla nyumbani kwake.

Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano wa Chadema, John Mrema alisema ni kweli Mbowe ameanguka ghafla na amepelekwa Muhimbili.

Chanzo: mwananchi.co.tz