Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkutano wakuu wa nchi EAC kujadili corona wakwama kufanyika

102595 Pic+eac+2 Mkutano wakuu wa nchi EAC kujadili corona wakwama kufanyika

Wed, 15 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Mkutano wa dharura wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) kujadili ugonjwa wa corona umekwama kufanyika leo Jumatano Aprili 15, 2020.

Mkutano huo ulikuwa ufanyike kwa njia ya video ukiwahusisha marais wa  nchi sita wanachama wa jumuiya hiyo ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Burundi na Rwanda.

Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Balozi Liberat Mfumukeko ametoa taarifa hiyo leo akibainisha kuwa kukwama kwa mkutano huo kumetokana na  

na Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir kuwa na majukumu mengine.

"Sudan Kusini hivi karibuni wameunda Serikali ya mseto hivyo bado wanajipanga na kwa mujibu wa mkataba wa jumuiya mkutano hauwezi kufanyika kama nchi moja haipo," amesema

Hata hivyo, mkutano wa mawaziri wa afya ulifanyika na kuelezwa kuwa kila nchi inaendelea vizuri katika mapambano dhidi ya corona.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement

"EAC tunaendelea kushirikiana na nchi wanachama kuhakikisha tunapambana na ugonjwa huu kwa kupunguza maambukizi zaidi na kufanikisha matibabu na kinga,” amesema.

Leo ni mara ya tatu mkutano huo unaahirishwa kutokana na mmoja wa viongozi kukosekana kwa sababu ya kukabiliwa na majukumu mengine.

Chanzo: mwananchi.co.tz