Fri, 13 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muuguzi Mkenya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Marsabit nchini Kenya, Anna Duba ameshinda Tuzo ya Muuguzi Bora Duniani katika hafla kuu iliyofanyika Dubai na kupokea kiasi cha Sh milioni 580.749 (Ksh27m).
Anakuwa Mkenya mwingine kunyakua Tuzo za juu za kaada baada ya Global Teachers kumtangaza Mwalimu wa Sayansi kutoka mashambani nchini Kenya mwaka 2019 kama Mwalimu Bora na kumtunza tuzo ya kiasi cha dola za marekani milioni 1 sawa na zaidi ya Sh bilioni 2.3.
Peter Tabichi alifahamika kwa kugawa zaidi ya theruthi tatu ya mshahara wake kwa wenye uhitaji.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live