Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mamia wajitokeza kufanyiwa uchunguzi homa ya ini

68512 Ini+pic

Sun, 28 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamejitokeza katika Hospitali ya Aga Kkhan kufanyiwa uchunguzi wa homa ya ini.

Leo Jumamosi Julai 27, 2019 Mwananchi limeshuhudia wakazi hao, wengi wakiwa wanawake wakijitokeza kwa wingi katika upimaji huo ikiwa ni siku moja kabla ya maadhimisho ya kimataifa ya kupambana na ugonjwa huo.

Akizungumza na Mwananchi leo daktari bingwa wa mfumo wa chakula na ini wa hospitali hiyo, Casmir Wambura amesema mwitikio wa watu umekuwa mkubwa mno.

Amebainisha kuwa walipanga kufanya uchunguzi huo kwa watu wasiozidi 400 lakini hadi kufika saa nne asubuhi  zaidi ya watu 800 wamejitokeza.

“Ni jambo ambalo limetupa imani kwamba elimu kuhusu ugonjwa huu imefika na watu wameanza kuelewa hatari yake kiasi cha kuwahi kuchunguza afya zao,” amesema Wambura.

Amesema asilimia 80 ya watu wenye ugonjwa huo duniani hawajitambui kwa kuwa hawajafanya uchunguzi wa afya wala kupata chanjo.

Pia Soma

Hatua hiyo imesababisha wagonjwa kwenda hospitali wakiwa katika hatua mbaya na matokeo yake kupoteza maisha.

Faida Haji, mkazi wa Kimara ni miongoni mwa waliojitokeza kuchunguza afya na kueleza kuwa  awali hakufahamu athari za ugonjwa huo.

Chanzo: mwananchi.co.tz