Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makamu wa Rais Samia amaliza tatizo la X-Ray hospitali ya Nyamagana

Makamu wa Rais Samia amaliza tatizo la X-Ray hospitali ya Nyamagana

Thu, 12 Dec 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mwanza. Changamoto ya ukosefu wa  mashine ya X ray lililokuwa likiikabili  Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, limepatiwa ufumbuzi baada ya Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia  Suluhu Hassan kuahidi kuinunua.

Samia ametoa ahadi hiyo leo Jumapili Desemba 8, 2019 baada ya kuweka mawe ya msingi ya wodi ya wanaume na jengo la huduma ya uzazi ya mama na mtoto linalojengwa na Taasisi ya Maendeleo ya Aga Khan kupitia mradi wake wa Impact.

Ametoa mashine hiyo baada ya Mganga Mkuu wa Jiji la Mwanza, Juma Mfanga kusema wagonjwa wanapata taabu hivyo kusababisha foleni katika hospitali za Rufaa za Sekoutoure na Bugando.

“Hili la X ray limeisha, hivyo kamilisheni majengo inaletwa hapa mara moja,” amesema.

Pia, Suluhu amewasisitiza wananchi kuwa na bima ya Afya ili kuwarahisishia katika gharama za matibabu pindi wanapoumwa.

Amesema Serikali inajitahidi kuboresha huduma za afya hivyo wananchi nao wanawajibu kuipunguzia mizigo mzito.

Awali akitoa Meneja Mradi wa Impact Edina Selestine alisema jengo la  hilo la mama na mtoto litagharimu Sh190. 6 milioni.

Amesema kulingana na uhaba wa wodi wazazi walikuwa wanazimika kulala watatu hadi wanne  ambapo kwa mwezi hospitali hiyo inaweza kuzalisha 650.

Naye Dk Mfanga alisema jengo la wodi ya wanaume litagharimu Sh1. 4 bilioni ambalo litakuwa na uwezo wa kubeba vitanda 101.

Chanzo: mwananchi.co.tz