Fri, 26 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Wanaume watatu nchini Zambia wamelazwa hospitali baada ya kunywa dawa za asili zinazodaiwa kuongeza nguvu za kiume.
Kiongozi wa mkoa, Chanda Kasolo, ameiambia BBC kuwa mara baada ya kunywa dawa hizo, walianza kutapika kitu ambacho kilisababishwa na mchanganyiko wa chakula, pombe na dawa hizo za asili.
Wagonjwa hao wapo katika kituo hiko cha kipindupindu na wanaendelea vizuri na matibabu, hata hivyo si wagonjwa wa kipindupindu bali walikunywa dawa ya kuongeza nguvu ya kufanya tendo la ndoa inayojulikana kama Mvubwe.
Chanzo: bongo5.com