Tue, 13 Apr 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Mbunge wa Kahama Mjini, Jumanne Kishimba (CCM), amesema ipo haja mtu asipopata matibabu hospitalini, apige simu polisi ili askari wawakamate watoa huduma kwa kushindwa kutoa huduma.
Amesema hayo leo Jumatatu Aprili 12, 2021 wakati akichangia Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano (2021/22 hadi 2025/26).
Aidha, Kishimba amehoji bungeni kuwa, kama kampuni za simu zinamkopesha mtu hadi Sh. 300,000 bila hata kumuona. Kwanini serikali isiruhusu mgonjwa atibiwe kwa mkopo hospitalini?
Chanzo: globalpublishers.co.tz