Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kilichomkuta aliemdanganya Waziri Gwajima "mimi ni field marshal, utafungwa wewe" (+video)

Video Archive
Thu, 14 Jan 2021 Chanzo: millardayo.com

Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima amekemea vikali tabia ya watumishi wa sekta ya Afya kudanganya na badala yake amewataka kuwa weledi katika utumishi wao ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Dkt. Gwajima amesema hayo jana wakati alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Nansio Ukerewe Mkoani Mwanza na kubaini kuwepo malalamiko ya uhaba wa dawa kutoka wananchi yaliyowasilishwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Cornel Magembe.

Aidha, Dkt. Gwajima ameshangazwa kusikia wagonjwa hawapewi Paracetamol lakini alivyotembelea stoo akakuta dawa hizo zipo.

Pia namna mnyonyoro wa dawa unavyoendeshwa katika Hospitali hiyo umemshangaza Dkt. Gwajima kwani inaonekana kuna uzembe na ubadhirifu mkubwa wa dawa na kusababisha hasara kubwa kwa Serikali.

Chanzo: millardayo.com