Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kifua kikuu hakitibiki kwa waganga wa kienyeji

61578 TB+PIC

Thu, 6 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Licha ya Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kwenda kwenye vituo vya afya na hospitali kupimwa pindi wanapoona dalili za kifua kikuu (TB), kuna baadhi huenda kwa waganga wa kienyeji kupata tiba.

Msanii wa ngoma za asili kutoka kikundi cha Mukikute jijini Dar es Salaam, Gota Ngogota ni miongoni mwa waliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji kupata tiba, akidhani amerogwa kabla hajagundua kama anaumwa TB.

Takwimu za Serikali zinaonyesha watu watatu hufariki dunia kila baada ya saa moja nchini kwa sababu ya TB  sawa na idadi ya watu 70 kila siku.

Akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa ushiriki wa wadau katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo unaojulikana kwa jina la  ‘Stop TB Partnership’ ulioandaliwa na Health Promotion Tanzania wakishirikiana na Serikali hivi karibuni,  Ngogota alisema aliamini amerogwa kwa sababu homa zilizokuwa zinamkumba hakujua zinasababishwa na nini.

“Zilianza dalili za kawaida tu, nikajua ugonjwa wa kawaida lakini baadaye nilishangaa napata joto kali, nakohoa mfululizo na usiku natoka jasho jingi sana nikajua nitakuwa nimerogwa siyo bure,” anasema Ngogota.

Ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa hivi karibuni inaonyesha kifua kikuu  ndiyo ugonjwa hatari zaidi wa kuambukiza duniani.

Pia Soma

Takwimu za Umoja wa Mataifa (UN) zinaeleza kuwa hivi sasa watu milioni 10.4 duniani kote wameambukizwa ugonjwa huo huku watu milioni 1.6 wakifariki dunia kila mwaka.

 

Kwa simulizi zaidi ya msanii huyo, soma Jarida la Afya kesho Ijumaa Juni 7, 2019 katika gazeti la Mwananchi.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz