Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenyatta akomaa na malaria

98665 Pic+kenyatta Kenyatta akomaa na malaria

Wed, 11 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Nairobi. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, ametangaza vipaumbele vinne vitakavyokuwa msingi wa juhudi za kutokomeza ugonjwa wa Malaria Afrika ifikapo mwaka 2030.

Kenyatta ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Marais wa Afrika wanaopambana na Malaria (African Leaders Malaria Alliance (ALMA), alieleza hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari jijini hapa.

Alisema pamoja na mafanikio makubwa katika vita dhidi ya ugonjwa huo kwa miaka 10 iliyopita, ni muhimu kutafuta na kupata rasilimali zaidi zitakazosaidia kutokomeza ugonjwa huo.

Alitaja vipaumbele hivyo kuwa ni matumizi ya dijitali na takwimu za mapambano ya Makaria, ushirikiano na mashirika ya kikanda ndani ya Afrika na makundi ya ushauri ya vijana.

Rais Kenytta alisema vipaumbele hivyo vitaleta mapinduzi makubwa, vitatafuta suluhu dhidi ya changamoto za mapambano ya kutokomeza ugonjwa huo.

Alisema changamoto hizo zinajumuisha ushiriki hafifu wa wanawake, watoto na vijana, uhaba wa fedha toka sekta za ndani, za umma na binafsi pamoja na tishio la kudumaa kwa michango ya wahisani.

Pia Soma

Advertisement
“Pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana, ili kuwa na Afrika Tunayoitaka kama ilivyoelezwa kwenye mpango wa 2063, tusijisahau, badala yake tutafute na kupata rasilimali zaidi zitakazotusaidia kutokomeza Malaria na kuokoa maisha,” alisema Rais Kenyatta.

Kamishina wa Masuala ya Jamii wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Amira El-Fadil, alisema vipaumbele hivyo vimeungwa mkono na Umoja wa Afrika.

Mtendaji Mkuu wa ushirikiano wa kutokomeza Malaria, Dk Abdourahmane Diallo alisema vipaumbele hivyo vikiongozwa na ubunifu na ushirikishwaji wa wadau wote ndio njia sahihi ya kufikia malengo ya kutokomeza ugonjwa huo.

Chanzo: mwananchi.co.tz