Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kampeni tokomeza dengue, kipindupindu kufanyika kesho Dar

61704 DENGUE+PIC

Sun, 9 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam imeagiza wananchi kutii kampeni ya usafi wa mazingira itakayofanyika kesho Jumamosi Juni 8, 2019 kwa lengo la kuangamiza magonjwa ya kipindupindu na homa ya dengue.

Kampeni hiyo inafanyika ikiwa ni siku nne tangu  kutolewa kwa takwimu zilizoeleza watu 3,495 waligundulika na ugonjwa wa homa ya  dengue na kati yao 3,333 na vifo vitatu ni kutoka katika jiji la Dar es Salaam, huku kipindupindu kikiua watu watatu na wengine 55 kulazwa.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Juni 7, 2019 Mganga Mkuu wa Mkoa Dk Yudas Ndungile amesema wakuu wa wilaya za jiji wataongoza shughuli hiyo.

"Jumamosi hii Juni 8 tunaanza kampeni ya usafi wa mazingira kuondoa magonjwa ya kipindupindu na homa ya dengue jijini Dar es Salaam, inawezekana kila Mwananchi akishiriki kesho wananchi wajitokeze kwa wingi kufanya zoezi hii," amesema Dk Ndungile.

Amesema shughuli hiyo itashirikisha wananchi katika maeneo husika lakini pia Mwananchi mmojammoja kufanya usafi katika kaya zinazomzunguka.

"Eneo la Kigamboni Mkuu wa mkoa (Paul Makonda) ataongoza katika soko la feri Kigamboni, Ilala waakuwa Jangwani na eneo la  Mchikichini, Temeke watakuwa Azimio hivyohivyo Kinondoni na Ubungo nawasihi wananchi wenyewe katika maeneo yao yanayowazunguka wafanye usafi," amesema Dk Ndungile.

Pia Soma

Amesema wananchi wanapaswa kufika katika ofisi za Kata kwa ajili ya kupata dawa za viuadudu ambako watapata majina ya mawakala walioidhinishwa na being elekezi ili waweze kupulizia maeneo yao.

Chanzo: mwananchi.co.tz