Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

KCMC yaanza upasuaji wa Mgongo, Ubongo, na Mishipa ya Fahamu

0004254456641155d282a7b65bd6f026 KCMC yaanza upasuaji wa Mgongo, Ubongo, na Mishipa ya Fahamu

Mon, 8 Feb 2021 Chanzo: habarileo.co.tz

HOSPITALI ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC), imeanza kutoa huduma ya upasuaji wa kibingwa wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu.

Matibabu hayo ya kibingwa KCMC inafanya kwa ushirikiano na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI).

Mkurugenzi mtendaji wa Moi, Dk Respicious Boniface amesema lengo la kuanzisha matibabu ya kibingwa KCMC ni kupunguza msongamano wa wagonjwa wanaopewa rufaa kwenda Moi na nchi za nje.

Amesema wamekuwa wakipokea rufaa nyingi kutoka Kanda ya Kaskazini na ushirikiano huo utasaidia kumaliza changamoto ya watu kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za kibingwa.

Kwa upande wa Daktari bingwa wa upasuaji wa mgongo, ubongo na mishipa ya fahamu, KCMC, Honest Massawe amesema hospitali hiyo ina uhitaji mkubwa wa wataalamu waliobobea wa magonjwa hayo kwa kuwa wagonjwa ni wengi wanaohitaji huduma hiyo.

Chanzo: habarileo.co.tz