Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

JKCI yapewa kifaa cha kubaini asilimia 95 ya magonjwa ya moyo

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) imepata msaada wa kifaa cha kupima moyo chenye uwezo wa kubaini asilimia 95 ya magonjwa ya moyo kwenye mwili wa binadamu.

Kitaa hicho kinachofahamika kitaalam kama Echo Machine kimetolewa na taasisi inayoshughulika na kuokoa maisha ya watoto wenye matatizo ya moyo ya Sach Canada.

Akizungumza leo Jumatano Mei 29, 2019 mkurugenzi wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi amesema  kifaa hicho kimekuja wakati muafaka kutokana na muda mrefu kushindwa kubaini matatizo ya moyo.

Amesema kinaweza kuhamishwa kutoka eneo moja kwenda jingine, kwamba kinaweza kupelekwa mikoani kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa huko.

Amebainisha kuwa kifaa hicho kina uwezo wa kubaini mtoto mwenye matatizo ya moyo tangu akiwa tumboni mwa mama yake.

“Watoto wengi wanazaliwa  wakiwa na matatizo ya moyo lakini kwa kifaa hiki mama mjamzito akichunguzwa kuanzia wiki ya 20, tatizo linaweza kubainika.”

Pia Soma

“Tunawashukuru wenzetu wa Canada wametusaidia, vifaa hivi tunavyo ila cha aina hii chenye uwezo wa kuhamishika ndio cha kwanza. Kitatumika kuwafikia Watanzania wa maeneo mbalimbali nchini,” amesema.

Mkurugenzi wa Sach Canada,  Marni Brinder Byk amesema wanatambua juhudi za JKCI katika kukabiliana na matatizo ya moyo na ndio sababu wamewapatia kifaa hicho.

Chanzo: mwananchi.co.tz