Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ifahamu mikoa mitano iliyoweza kudhibiti malaria zaidi

8f83b8429372e85553643be8258b7ab1 Ifahamu mikoa mitano iliyoweza kudhibiti malaria zaidi

Thu, 11 Mar 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MIKOA mitano imepiga hatua katika kutokomeza ugonjwa wa Malaria nchi ambapo imetajwa kuwa na kiwango chini ya asilimia moja.

Mikoa iliyotajwa ni Kilimanjaro, Njombe, Arusha, Iringa na Manyara.

Akizungumza katika kikao kazi cha kwanza cha Wabobezi wa kudhibiti wadudu wanaoeneza magonjwa, Mkurugenzi wa Idara ya Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Leonard Subi alisema kuwa mikoa mingine ina kiwango cha kati cha maambukizi hayo ya malaria.

Aidha, Dk Subi alisema pia wapo nzi weusi ambao wanaeneza ugonjwa wa usubi hususani kwenye mikoa ya Mbeya (Tukuyu), Morogoro (Mahenge) na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Iringa.

Chanzo: www.habarileo.co.tz