Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hospitali ya Aga Khani yatangaza neema kwa wanawake, watoto Tanzania

Mon, 10 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam imesema kambi ya kutoa huduma ya upasuaji wa kubadili na kuboresha maumbile au ngozi iliyokakamaa kwa wanawake na watoto wa kike masikini itafanyika mara mbili mwaka 2019 badala ya mara moja kama iliyokuwa miaka minne iliyopita tangu kuanzishwa kwake.

Kambi hiyo inalenga kuwasaidia wanawake na watoto wa kike maskini wenye ulemavu  uliosababishwa  na ukatili wa nyumbani, kuungua  na ajali na matibabu yake yanatolewa bure.

Akizungumza na wanahabari leo Jumatatu, Juni 10, 2019  Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Aidan Njau amesema awamu ya kwanza itaanza mwezi huu na inayofuata itafanyika Agosti.

"Kumekuwa na mwitikio mkubwa katika kambi hii na matunda yake yameonekana ndio maana tumeamua tufanye mara mbili kwa mwaka huu ili kuwapa fursa ya kupata huduma za matibabu haya. katika awamu zote mbili tunatarajia kuwafikia wanawake na watoto kike takriban 100,” amesema Dk Njau

"Shughuli hii tutaifanya tukishirikiana na madaktari bingwa kutoka Muhimbili (Hospitali ya Taifa), Marekani na Aga Khan. Ushirikiano huu unalenga kuimarisha utaalamu wa upasuaji kwa ajili ya kushughulikia hitiji la tiba ya upasuaji wa kubadili na kuboresga maumbile," amesema

Dk Njau amefafanua kambi kubwa ya uchunguzi wa kuwatambua wagonjwa wengine uhitaji wa matibabu hayo utafanyika katika Hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam na vituo vyake vya afya vilivyopo mikoa ya Mwanza, Mbeya, Dodoma,  Tabora, Bukoba, Tanga, Iringa na Morogoro, kuanzia Juni 15.

Pia Soma

Mkuu wa Kitengo cha Upasuaji cha Hospitali Aga Khan, Dk Athar Al amesema tangu kuanzishwa kwa kambi hiyo mwaka 2016 jumla ya wanawake na watoto 143 wamenufaika na mpango huo na kuwa na mwonekano mzuri.

"Upasuaji huu ni gharama sana kwa mtu mmoja anaweza akalipia Sh 5milioni kwa ule upasuaji mkubwa wakati mdogo analipia Sh 2milioni, lakini kupitia kambi hii tunatoa bure huduma tukishirikiana na wadau mbalimbali," amesema Dk Al.

Chanzo: mwananchi.co.tz