Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Homa ya dengue yaua wawili, wagonjwa waongezeka Dar es Salaam

55839 Pic+dengue

Mon, 6 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Zikiwa zimepita siku 24 tangu Serikali itangaze kuwapo kwa homa ya dengue nchini, watu 1,222 wamegundulika kuugua ugonjwa huo jijini Dar es Salaam, Tanga na Singida huku wawili wakifariki dunia.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya, Aprili 12 watu 307 waligundulika kuwa na homa hiyo.

Akizungumza jana, Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile alisema kasi ya kukua kwa ugonjwa huo imeongezeka, “mpaka sasa, takwimu tulizonazo, Mkoa wa Dar es Salaam unaongoza kwa kuwa na wagonjwa 1,145, Tanga tumepata wagonjwa 76 na Singida tumepata mgonjwa mmoja, lakini pia kuna vifo viwili vimetokea.” Takwimu hizo ni zile zilizokusanywa kuanzia Januari Mosi hadi Ijumaa iliyopita katika hospitali za umma na binafsi nchini.

Kuhusu mikakati ya Serikali kudhibti ugonjwa huo, Dk Ndugulile alisema vitendanishi kwa ajili ya uchunguzi vimeshawasili nchini na pia wizara imeshaziagiza halmashauri kuhakikisha zinanunua viuatilifu na kupuliza katika maeneo yote yanayopaswa.

“Rais John Magufuli alishatoa maelekezo, kila halmashauri inatakiwa kutenga fedha kwa ajili ya kununua viuatilifu na kusambaza katika maeneo yote ili kuua mazalia ya mbu na wadudu wengine, tunachokifanya sasa ni kuhamasisha wananchi wenyewe kuchukua hatua ikiwamo kujikinga kwa kutoweka maji yaliyotuama ndani, kuondoa mazalia ya mbu na kufyeka nyasi,” alisema.

Aidha, imelezwa kuwa dawa zote zenye diclofenac si salama kwa mgonjwa mwenye homa ya dengue ambazo ni Ibuprofen, Brufen na Diclopar.

Habari zinazohusiana na hii

Mtafiti wa tabia za mbu kutoka Taasisi ya Afya ya Ifakara (IHI), Dk Nicholaus Govela alisema mbu anayeambukiza homa ya dengue ni Aedes Egypti na hawezi kubeba vimelea vya malaria na anayeambukiza malaria hawezi kuambukiza dengue kutokana na maumbile yao. Dk Govela alisema fiziolojia ya mwili wa mbu haiwezi kuruhusu Aedes kubeba virusi vya mbu mwingine, “ndiyo maana mbu hawezi kuambukiza Virusi vya Ukimwi (VVU).”

Alisema mbu wa dengue aina za Aedes Egypti, Aedes Albokictus na Aedes Africans, huuma mchana.



Chanzo: mwananchi.co.tz